1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MichezoBrazil

Rais Lula akosoa uteuzi wa Carlo Ancelotti kuinoa Brazil.

7 Julai 2023

Siku chache baada ya shirikisho la soka nchini Brazil kumtangaza kocha Carlo Ancelotti kuwa atabeba mikoba ya kuinoa timu ya taifa hilo mwakani, Rais wa nchi hiyo ameibuka na kuukosoa uamuzi huo.

https://p.dw.com/p/4Tabm
Frankreich, Paris | Lula da Silva beim Power Our Planet
Rais wa Brazil Lula da Silva .Picha: Stephanie Lecocq/REUTERS

 
Rais wa Brazil  Lula da Silva aukosoa uteuzi wa Carlo Ancelotti kuwa kocha mkuu wa timu yataifa ya Brazil.

Siku chache baada ya shirikisho la soka nchini Bazil CBF kumtangaza Carlo Ancelotti kuwa kocha mkuu wa timu ya taifa ya Brazil kuanzia mwaka 2024, Rais wa Brazil Luiz Inacio Lula da Silva amekosoa uteuzi wa Carlo Ancelotti kama kocha mpya wa kandanda wa Brazil, akidai angekuwa bora zaidi kutatua matatizo ya timu ya taifa ya Italia.

 

Soma zaidi: Brazil yamtangaza Carlo Ancelotti kuwa kocha mkuu wa timu ya taifa kuanzia mwaka 2024

Muitaliano Ancelotti, ambaye ameshinda rekodi ya Ligi ya Mabingwa ulaya mara nne kama kocha, atachukua mikoba kabla ya michuano ya Copa America nchini Marekani mwezi mwaka ujao mara tu baada ya kutimiza mwaka wa mwisho wa mkataba wake na Real Madrid.

Fußball | Valencia CF v Real Madrid CF - LaLiga Santander
Kocha wa Real Madrid Carlo Ancelotti atachukua mikoba ya timu ya taifa ya Brazil selecao mwakani.Picha: Jose Breton/NurPhoto/picture alliance

 Rais Lula amesema   "Ninampenda Ancelotti, lakini hajawahi kuwa kocha wa timu ya taifa ya Italia, Kwa nini hatasuluhishi tatizo la Italia, ambao hawakufuzu kwa Kombe la Dunia la 2022?" aliongeza Rais huyo mwenye umri wa miaka 77. Kwa muda, kocha wa Fluminense Fernando Diniz atakuwa kocha wa Brazil kwa mechi yao ya ufunguzi ya kufuzu kwa Kombe la Dunia la 2026.


“Mimi ni shabiki wa Diniz,” alisema Lula. "Ana utu, ubunifu na ndiye anayeamuru chumba cha kubadilishia nguo."


Shirikisho la Soka la Brazil (CBF) limemchagua Ancelotti mwenye umri wa miaka 64 likiamini kuwa mmoja wa makocha waliofanikiwa zaidi katika historia ya soka barani Ulaya atawakabidhi kombe lao la sita la Kombe la Dunia lakini la kwanza tangu 2002.

Italien Nationalmannschaft Brasilien Training in Turin
Wachezaji wa timu ya taifa ya Brazil maarufu Selecao wakiwa mazoezini .Picha: Nderim Kaceli/IMAGO

Soma zaidi :China na Brazil zakubaliana kuimarisha uhusiano

 Hamu hiyo ni kubwa zaidi baada ya wapinzani wao Argentina kushinda huko Qatar Desemba mwaka jana ambapo Brazil ilitolewa katika robo-fainali na kocha wake Tite nani kujiuzulu.

 Ancelotti atakuwa kocha wa nne ambaye si Mbrazil kufundisha timu ya taifa Brazil. Wa mwisho alikuwa Muajentina Filpo Nunez ambaye alisimamia mchezo mmoja mnamo 1965.