1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroHaiti

Watetezi wa haki waiomba Marekani kutowarudisha Wahaiti

28 Machi 2024

Karibu mashirika 500 ya kutetea haki za binadamu na uhamiaji yamesaini barua inayotoa wito kwa serikali ya Marekani kusitisha hatua ya kuwarudisha nyumbani raia wa Haiti.

https://p.dw.com/p/4eDRQ
Hali inavyoonekana katika baadhi ya viunga vya Haiti kufuatia vurugu za magenge ya wahalifu
Mji mkuu wa Haiti, Port-au-Prince umegubikwa na machafuko ya magenge ya wahalifu na kusababisha baadhi ya raia kukimbia taifa hilo.Picha: Guerinault Louis/Anadolu/picture alliance

Shirika lisilo la kiserikali la Haitian Bridge Alliance, lenye makao yake San Diego, hapo jana lilichapisha barua pamoja na mashirika mengine 481 yakiitaka Marekani kuongeza hali ya ulinzi wa muda kwa Wahaiti, isitishe kuwarudisha nchini mwao kwa lazima, iwaachie wahamiaji waliokamatwa na kutanua mipango ya kuwasamehe wakimbizi.

Nchi kama Marekani, Canada na Ufaransa zimekuwa zikiwaondoa raia wao na wafanyakazi wa mashirika kama Umoja wa Mataifa, Umoja wa Ulaya, Benki ya Dunia na Shirika la Fedha Duniani IMF kutoka nchini humo.

Mataifa jirani ya Haiti kwa upande wao yamekuwa yakiongeza ulinzi katika mipaka yao na kuwarejesha nyumbani Wahaiti wanaokimbia machafuko, hatua ambayo imelaaniwa na Umoja wa Mataifa.