1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

IOM yataka dola bilioni 7.9 kusaidia wahamiaji

Lilian Mtono
22 Januari 2024

Shirika la Wahamiaji la Umoja wa Mataifa (IOM) kwa mara ya kwanza limetoa ombi kwa jamii ya kimataifa ya dola bilioni 7.9 kwa ajili ya kuwasaidia watu wanaohama na kuhakikisha njia salama kwa wahamiaji.

https://p.dw.com/p/4bY0n
Wahamaji, Shirika la Umoja wa Mataifa la Wahamiaji, IOM, Addis Ababa, Ethiopia.
Wahamaji kweye kituo cha Shirika la Umoja wa Mataifa la Wahamiaji mjini Addis Ababa, Ethiopia.Picha: Michele Spatari/AFP

Ombi hili linatolewa wakati changamoto kama za mabadiliko ya tabianchi, mizozo na hali mbaya za kiuchumi na fursa vikisababisha mamilioni ya watu kukimbia makazi yao.

Ombi hili la mwaka linalifanya shirika hilo sasa kusaka zaidi ufadhili kwa ushirikiano na mashirika mengine ya Umoja wa Mataifa na makundi ya kibinaadamu, katika wakati ambapo wafadhili wengi wakubwa wakikabiliwa na changamto za kibajeti ama kupunguza matumizi ya misaada.

Lakini IOM yenyewe imesema wanatumaini ufadhili mkubwa utatoka kwa watu na sekta binafsi pamoja na serikali

Ombi hili ni sehemu ya mpango mkakati wa miaka mitano chini ya mkurugenzi mpya wa IOM Amy Pope na utawanufaisha watu milioni 140, wahamiaji na jamii zinazowapokea.